• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

ENDELEZENI MABOMA YASIYOISHA..

Posted on: June 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alhaj Abubakari Kunenge ameiagiza Halmashauri ya Bagamoyo,kuhakikisha inayaendeleza maboma ya miradi iliyokwama yenye thamani ya Bilioni 1.2 ,kwani kwa kuendelea kubaki viporo ni hasara kwa Serikali.

Aidha ameitaka Halmashauri hiyo kutumia raslimali zilizopo kwenye uchumi wa bluu na historia za kale ili kukuza Uchumi wake ambao bado unatakiwa kufanyiwa kazi maalum.

Kunenge alitoa maagizo hayo katika kikao cha Baraza la halmashauri maalum la kupitia hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Kunenge alieleza ,agizo hilo sio kwa Halmashauri ya Bagamoyo pekee bali kila Halmashauri ya mkoa huo ,zijipange kukamilisha miradi yote viporo ili ilete tija ndani ya jamii.

Alielezea,kupata hati safi kuendane na utekelezaji wa vipaombele vyenye tijà vitakavyotatua kero za wananchi pamoja na kukamilisha miradi iliyotengewa mabilioni ya fedha kutoka Serikalini.

“Miradi inakuja kuleta jibu kwa Wananchi, miradi ya toka mwaka 2015 ,haijakamilika hadi leo,hii ni hasara kwa Serikali,tengeni fedha za mapato ya ndani kukamilisha baadhi ya miradi hii, mkiiacha miradi Kuwa maboma mnachelewesha maendeleo ya wananchi,” Naziagiza Halmashauri zote kutekeleza miradi hiyo ya wananchi ilete tija badala ya kujivunia hati safi kila mwaka “alisisitiza Kunenge.

Vilevile, Kunenge alimuagiza Katibu Tawala mkoa wa Pwani, Rashid Mchatta pamoja na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, kufanya kazi maalum kwani kuna fursa nyingi kwenye uchumi wa bluu na kutumia historia za kale ili kujiinua kimapato.

” Bagamoyo Ina fursa za kihistoria ,uchumi wa bluu ,lakini bado inahitajika nguvu ya kufanyia kazi madhubuti kuinua uchumi uliopo .”

Mkuu huyo wa mkoa, alihimiza kutafuta vyanzo vipya vya mapato na kufanyia uchambuzi vyanzo vilivyopo ambavyo havifanyi vizuri kuongeza mapato ili visimamiwe na kuwekewa nguvu viweze kufanya vizuri.

“Tafuteni vyanzo vipya vya mapato.
Nawaagiza watendaji wa Halmashauri kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ili kuisaidia Serikali kutimiza majukumu yaliyopo kwa wakati”

Mkaguzi Mkuu wa nje kutoka ofisi ya CAG Mkoa wa Pwani Mary Dibogo alieleza ,Halmashauri zihakikishe zinaepuka kuzalisha hoja.

Alizitaka pia zikamilishe miradi ya kipindi kirefu ikiwemo wilaya ya Bagamoyo ambayo haijakamilisha miradi yenye thamani ya Bilioni 1.2, sanjali na Chalinze miradi yenye thamani ya Bilioni 2.3 na Kisarawe miradi iliyoanzishwa haijakamilishwa ya Bilioni 2.2.

Dibogo alisema, fedha zinatengwa na Serikali ili kutekeleza miradi na kama ikiwa haitoshelezi Lazima ipatiwe namna ya kuikamilisha .

Awali Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo Mohammed Usinga alieleza, kulikuwa na hoja 35, kati ya hizo 18 zimefutwa na 17 bado hazijafungwa.

Usinga alimuhakikishia ,mkuu wa mkoa wa Pwani kwamba, Halmashauri hiyo itafanyia kazi maagizo na maelekezo yote.




Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRATIBU WA MRADI WA MARCOSIO TAFIRI AONGOZA WASHIRIKI WA WARSHA KUTEMBELEA WAVUVI WILAYA YA BAGAMOYO...

    May 29, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI...

    May 23, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA UCHAGUZI AKAGUA MWENENDO WA UANDIKISHAJI...

    May 18, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA MAZUNGUMZO NA BODI YA UTALII..

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo