• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

PERI URBAN YAWAKA BAGAMOYO

Posted on: August 7th, 2019

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Hamisi Mgalu,amezindua Mradi wa Usambazaji Umeme katika Vijiji vilivyopo Pembezoni mwa Miji (Peri-Urban Rural Electrification Program) wilayani Bagamoyo ikiwa ni muendelezo wa uzinduzi wa miradi hiyo nchi nzima.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Naibu waziri huyo wa Nishati amesema lengo la serikali ni kuwasha umeme katika vijiji 10,278 ifikapo mwezi Juni 2020, ambapo mpaka sasa vijiji 7,349 tayari vimeshaunganishwa umeme.

Alisema katika mradi huo wanachi elfu sita wa awali wataunganishiwa umeme katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kata za Magomeni, Kerege, Zinga, Kiromo Mapinga na vitongoji vyake katika Halmashauri ya Bagamoyo.

Aliongeza kwa kusema kuwa, hayo yote yanatekelezwa kutokana na uongozi mzuri wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, kusimamia ukusanyaji wa kodi ili fedha zielekezwe kwenye miradi ya maendeleo kama hiyo.

Naibu waziri huyo wa Nishati ametumia nafasi hiyo kuwaagiza wakandarasi na wasambazaji na wazalishaji  wa vifaa vinavyotumika kwenye miradi ya umeme kuzalisha vifaa vyenye ubora ili miradi inayojengwa iwe ya kudumu.

Aidha, alisema wakandarasi wanapaswa kutumia vifaa vinavyozalishwa na kampuni za ndani ili kuongeza pato la ndani kutokana na kodi za wenye viwanda hivyo.

Nao wasambazaji wa vifaa hivyo wametakiwa kuacha urasimu na badala yake wafanye kazi kwa kuzingatia weledi wa kazi yao kulingana na mahitaji ya wakandarasi ili vifaa viwafikie wakandarasi kwa wakati nao waweze kutekeleza miradi ndani ya kipindi cha mikataba yao.

Alitoa onyo kwa yeyote atakaejaribu kumkwamisha mkandarasi, kuwa hatua hiyo ni kukwamisha juhudi za wizara, na ukiikwamisha wizara umemkwamisha Rais wa Jamuri ya Muungano wa Tanzania na kwamba utakuwa ni miongoni mwa wanaorudisha maendeleo nyuma na serikali haitokuvumilia.

Awali akizungumza mbele ya Naibu waziri, Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi, Amos Maganga, amesema mradi huo utagharimu shilingi Bilioni 12 . 8 utakapokamilika.

Nae Mbunge jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Kawambwa, amesema anamshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo mradi huo ndani ya jimbo lake.

Aidha, amempongeza waziri wa Nishati Medard Kalemani pamoja na Naibu waziri Subira Mgalu kwa kazi kubwa wanayofanya ya kusimamia vyema miradi ili itekelezwe ndani ya wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • WAPENI ELIMU WANANCHI KUHUSU UGOJWA WA MPOX...

    March 17, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo