• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA MAKUNDI MBALIMBALI ILI YAFAHAMU MALENGO YA SADC.

Posted on: July 25th, 2022

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema kuwa, itaendelea kushirikiana na makundi mbalimbali katika jamii vikiwemo vyombo vya habari ili kuhakikisha wanayafahamu malengo na mikakati ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) waweze kuibua fursa mbalimbali zilizopo katika nchi wanachama kwa lengo la kuwashirikisha Watanzania waweze kuzitumia kujiendeleza.

Hayo yamesemwa leo Julai 25, 2022 na Balozi Agnes Kayola wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine katika ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa wanahabari mjini Bagamoyo mkoani Pwani yanayoratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).

Lengo la warsha hiyo ni kuwajengea uelewa wanahabari kuhusu Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ili waweze kushiriki kikamilifu kutoa taarifa chanya ambazo zitakuwa na hamasa kwa Watanzania waweze kuzitambua fursa zilizopo katika jumuiya hiyo.

“Tanzania ni miongoni mwa nchi waanzishi wa SADC ambayo ina umri wa miaka 40. Waandishi wa habari mna mchango mkubwa kuhakikisha kundi la vijana linafahamu ipasavyo umuhimu wa SADC ili waweze kushiriki na kuzitumia fursa zilizopo katika jumuiya hii ya kikanda kwa manufaa,”amesema Balozi Kayola.

Amesema, licha ya fursa nyingi zilizopo katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo, pia Tanzania inazo huduma nyingi ambazo zikitumika ipasavyo zitaweza kuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa jamii na Taifa kwa ujumla.

“Pia kutokana na fursa zinazopatikana tutaendelea kutumia lugha yetu ya Kiswahili kama bidhaa, hivyo jukumu kubwa ambalo mnapaswa kulifahamu ni kuhakikisha mnakitumia Kiswahili ipasavyo katika kutoa taarifa zenu,”amesema.

Amefafanua kuwa, malengo ya SADC kama ilivyoelezwa katika Kifungu cha 5 cha Mkataba wa SADC (1992) ni kufikia maendeleo ya kiuchumi, amani na usalama, na ukuaji, kupunguza umaskini, kuimarisha kiwango na ubora wa maisha ya watu wa Kusini mwa Afrika.

Sambamba na kusaidia watu wasiojiweza kijamii kupitia Ushirikiano wa Kikanda. “Malengo haya yanapaswa kufikiwa kwa kuongezeka kwa Mtangamano wa Kikanda, unaojengwa kwa misingi ya kidemokrasia, na maendeleo yenye usawa na endelevu,”amesema.

Balozi Kayola amesema kuwa, kupitia SADC wana mikakati mbalimbali ikiwemo kuwaenzi viongozi waanzilishi akiwemo Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

“Kwa kuzingatia hilo sanamu ya Mwalimu Nyerere itajengwa kwenye jengo la amani na usalama huko Addis Sababa nchini Ethiopia, mkakati huo unaendelea,”amesema.

Pia amesema, jukumu lingine walilonalo ni kuhamasisha jamii ya Watanzania waaweze kufahamu kuhusu majukumu, malengo na fursa zinazopatikana kwenye jumuiya ya SADC.

LENGO LINGINE NI KUHAMASISHA UMOJA NA USHIRIKIANO KATIKA NCHI WANACHAMA, KWA KULIZINGATIA HILO MHESHIMIWA DKT.JAKAYA KIKWETE,RAIS MSTAAFU WAA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ALITEULIWA KUWA MWENYEKITI WA JOPO LA WAZEE WA JUMUIYA YA MAENDELEO KUSINI MWA AFRIKA (SADC), LINALOSHUGHULIKIA MIGOGORO KATIKA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA,”AMESEMA BALOZI KAYOLA.

Amesema, lengo lingine ni kutoa elimu kuhusu mtangamano wa jumuiya hiyo na ushiriki wa sekta ya habari katika kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kufikisha taarifa chanya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • WAPENI ELIMU WANANCHI KUHUSU UGOJWA WA MPOX...

    March 17, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo