• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

TUMIENI NISHATI MBADALA...

Posted on: May 16th, 2023


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa( 2023) ,Abdallah Shaib amehimiza wananchi kuongeza matumizi ya Nishati Mbadala (gesi) ,badala ya kutumia mkaa na kuni ambao huchochea ongezeko la ukataji miti kiholela.

Alitoa msukumo huo ,katika Mbio za Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Bagamoyo,wakati akipokea taarifa na kukagua shughuli za mabadiliko ya tabia nchi, hifadhi ya Mazingira na Utunzaji wa Vyanzo vya maji -upandaji wa miti, Shule ya Sekondari Hassanal Damji, pamoja na kugawa mitungi ya gesi kwa baadhi ya mama lishe kata ya Magomeni Wilayani humo.

Kiongozi huyo aliitaka Jamii,kushirikiana na Serikali kupambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Shaib alisema, matumizi ya Nishati mbadala ni agenda ambayo itaokoa raslimali za misitu na kimsingi ni muokozi wa maisha yetu .

Aidha anazisisitiza, Sekretariet za Mikoa na Halmashauri za wilaya, kusimamia sheria,kanuni na miongozo inayotolewa na Serikali kuhusu uhifadhi wa Mazingira,misitu na raslimali zake, Vyanzo vya maji na maeneo tengefu.

Shaib alizitaka pia kusimamia sheria ndogo ndogo zinazotungwa na Halmashauri hizo kwa lengo la kuhifadhi Mazingira,usafi na vyanzo vya maji.

Sambamba na hayo, ziandae bajeti ndogo ambazo zitaongeza nguvu katika udhibiti wa Utunzaji wa Mazingira.

Hata hivyo alisema, kwa zaidi ya asilimia 95 matendo ya shughuli za kijamii yanapelekea kuharibu Mazingira hali ambayo inaenda kuharibu ikolojia ya viumbe hai na uchumi wa Taifa.

“Ukataji wa miti usiozingatia Utunzaji wa Mazingira,hupelekea upotevu wa bioanuai ikiwemo wanyama na mimea, ardhi kupoteza rutkwauba kupungua kwa pato la Taifa linalotokana na utalii, kupungua kwa kipato cha kaya zinazotegemea raslimali za misitu kupungua kwa raslimali zitokanazo na misitu na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabia nchi.”

Vilevile, Shaib alitaka jamii kuepuka matumizi ya taka ngumu,vifungashio vya plastic ambavyo kwa kiasi kikubwa vinaharibu Mazingira.

Pia ufugaji kwa kukusanya makundi makubwa ya mifugo pamoja na uchimbaji madini holela pamoja na kuzuia uvuvi haramu.

Ofisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, James Chui alisisitiza Halmashauri zote kutekeleza maagizo ya kupanda miti milioni 1.5 kwa mwaka sanjali na kutoa elimu ya upandaji miti kwa jamii.

“Katika Mbio za Mwenge wa Uhuru kila mradi tunaopita tunahakikisha miti 500 inapandwa kwenye kila Halmashauri na zinatakiwa kufuata maelekezo hayo” anaeleza Chui.

Mapema Mei 16 , Mwenge wa Uhuru ulipokelewa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo ukitokea Halmashauri ya Chalinze,ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Shauri Selenda alieleza, Mwenge huo utapitia miradi Tisa yenye thamani ya sh.Bilioni 2.3.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • WAPENI ELIMU WANANCHI KUHUSU UGOJWA WA MPOX...

    March 17, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo