• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

VITONGOJI 6 BAGAMOYO KUTOSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2019

Posted on: September 18th, 2019

VITONGOJI Sita vilivyopo maeneo ya uwekezaji kata ya Zinga pamoja na RAZABA kata ya Makurunge eneo la serikali alilopewa mwekezaji BAKHRESA kwa ajili ya uwekezaji wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani vimefutwa kwa mujibu wa sheria na havitoshiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020.


Vitongoji hivyo ni Kikonga ,Kasiki ,Pande ,Mkunguni, Mbegani vilivyopo kata ya Zinga eneo la EPZA na RAZABA kata ya Makurunge .


Akizungumza katika baraza la madiwani, Bagamoyo mkuu wa wilaya hiyo, Zainab Kawawa aliwaasa madiwani na viongozi kwenye maeneo hayo wasijiingize katika ushabiki wowote kutokana na maamuzi hayo ya serikali ambayo ni ya msingi na yenye nia njema.


Alieleza ,vitongoji hivyo vimefutwa na Tume ya Uchaguzi ,na mchakato huo ulianzia chini ,msije kukosoa na kupingana na serikali na kushirikiana na wananchi ambao wameshaanza kunung'unika .


"Uchaguzi unatarajiwa kuwa Novemba 24 mwaka huu, madiwani mtoe ushirikiano katika maandalizi ya uchaguzi huo ,ili kupata viongozi bora,"


"Msipange safu ,kwani itasababisha kupata viongozi wasio bora,tunataka uchaguzi uwe huru na wa haki na usio na chembe ya rushwa"alifafanua Zainab .


Nae msimamizi wa uchaguzi , wilaya ya Bagamoyo, Malboard Kapinga alieleza kwamba, uchaguzi huo hautohusisha vitongoji hivyo sita kutokana na wananchi kulipwa fidia kwenye maeneo ambayo yapo katika uwekezaji na walitakiwa kuondoka.


Kapinga alibainisha ,bajeti ya uchaguzi itagharimu takriban milioni 200 ambapo serikali kuu itatoa milioni 163 na halmashauri milioni 54 na hadi sasa serikali kuu imeshatoa milioni 119 na halmashauri milioni 27.


"Elimu ya uraia tunatarajia kuendelea kuitoa mwezi octoba katika maeneo yote vitongoji 167 na vijiji nane na vifaa vya uchaguzi vimeanza kuandaliwa"aliweka bayana.


Awali diwani wa viti maalum kata ya Yombo Elizabeth Shija alilitaka kundi la wanawake kujitokeza kushiriki kugombea nafasi mbalimbali za uchaguzi na kuwaasa kuthubutu bila uoga ili kufikia 50 kwa 50.


Diwani wa kata ya Yombo ,Muhammed Usinga alisema wamejipanga na tayari wamehamasisha wanaCCM kuanzia ngazi ya tawi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wakazi.


Alisema ,hakuna asiyekosa macho ama kusikia ,utekelezaji wa ilani ya CCM umetekelezeka kwa asilimia kubwa chini ya Rais dkt.John Magufuli na hakuna wakumpinga kutokana na juhudi zake za kuinua maendeleo na uchumi kijumla.


Usinga ,aliwaomba wananchi wasifanye makosa katika uchaguzi huo na uchaguzi mkuu 2020 ,wachague CCM ili kuendelea kula matunda .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • BAGAMOYO KUJITANGAZA KIMATAIFA SEKTA YA UTALIII...

    May 10, 2025
  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo