• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

WAFANYABIASHARA TUMIENI BANDARI YA BAGAMOYO : DC KAWAWA

Posted on: June 3rd, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mhe. Zainab Kawawa amewasihi wafanyabiashara kutumia bandari ya Bagamoyo kuingiza bidhaa zao na kusafirisha bidhaa zinazotoka nje ya Bagamoyo.

Mhe. Zainab ameyasema hayo alipofanya mkutano maalum na wafanyabiashara wa Bagamoyo wanaotumia bandari ndogo ya Bagamoyo baada ya wafanya biashara hao kuacha kutumia bandari hiyo wakidai huduma zisizoridhisha toka kwa uongozi wa mamlaka ya bandari ya Bagamoyo.

Akizungumza kwa niaba ya Wafanyabiashara wanaotumia bandari ya Bagamoyo, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara hao Bw. Shabani Khamsini Almaarufu “Chavurugu” amesema, Uongozi wa Mamlaka ya bandari ya Bagamoyo umekuwa ni kero kwa wafanyabiashara kwani baadhi ya Maofisa Bandari wamekuwa na lugha chafu za matusi kwa wafanyabiashara hao, kutoa risiti zenye kiwango tofauti na pesa wanazolipia huduma, na wakati mwingine kutishia kuwapiga wanapofika Ofisi za bandari kupata ufafanuzi na huduma, Amesema Mwenyekiti huyo.

Baada ya kupokea kero na malalamiko ya wafanyabiashara hao Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo amesema ni kinyume cha kanuni, taratibu, sheria na miongozo ya Utumishi wa umma kwa Mtumishi kutoa lugha chafu kwa wateja anaowahudumia, kuwapiga na kuhujumu mapato ya Serikali kwa kutoa risiti inayotofautiana na kiasi cha fedha alichopokea, hivyo akawataka wafanyabiashara hao kuhakikisha tuhuma walizowasilisha kwake zina ukweli kwani mara baada ya mkutano huo kamati ya Ulinzi na usalama itaanza uchunguzi wa tuhuma hizo mara moja ili sheria ichukue mkondo wake kwa Maofisa wote wanaohusika na ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa umma, maana vitendo hivyo vimeiingizia Serikali hasara kubwa baada ya wafanya biashara hao kuisusa bandari ya Bagamoyo na kuacha kabisa kuingiza bidhaa kupitia bandari ya Bagamoyo.

“Naombeni rudini itumieni bandari ya Bagamoyo, ni mali yenu, ni kwa ajili yenu, chonde chonde rudini mtumie bandari yenu kibiashara, nipo pamoja nanyi kusimamia haki zenu na maslahi yenu na nawaahidi kufuatilia na kumaliza kero na malalamiko yenu yote na wote wanaohusika katika kuwakwamisha ntahakikisha wanachukuliwa hatua stahiki,” Amesema Mhe. Zainab Kawawa.

Aidha Mhe. Zainab Kawawa ametumia mkutano huo kumwagiza Meneja Bandari ya Bagamoyo Bw. Witharo Jared Witharo kuacha mara moja vitendo anavyoshutumiwa navyo vya ukiukwaji wa maadili, kanuni, sheria na taratibu za Utumishi wa umma na ahakikishe anatoa huduma bora kwa wafanya biashara hao ili kurejesha hadhi ya bandari hiyo kama ilivyokuwa mwanzo.

Bandari ya Bagamoyo imepata mtikisiko mkubwa wa kimapato baada ya mapato yanayotokana na bandari kushuka kutoka Shilingi Bilioni 03 Mwezi Novemba Mwaka 2019 hadi kufikia Shilingi Milioni 293.8 Mwezi Mei mwaka huu baada ya wafanyabiashara wanaotumia bandari hiyo kususia kuingiza mizigo kupitia bandari ya Bagamoyo wakilalamikia usumbufu mkubwa na huduma mbovu zilizokuwa zikitolewa kwenye bandari hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • BAGAMOYO KUJITANGAZA KIMATAIFA SEKTA YA UTALIII...

    May 10, 2025
  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo