• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

WANANCHI CHANGIENI SHUGHULI ZA MAENDELEO- RC NDIKILO

Posted on: February 6th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Eng. Evarist Ndikilo amefanya ziara maalum ya kutembelea, kukagua na kuhimiza Wananchi kushiriki shughuli za maendeleo hususani kuchangia ujenzi wa madarasa ya Shule za Sekondari.

Ziara hiyo ya siku moja iliyoanzia katika Kata ya Mapinga ambapo Mkuu wa Mkoa alipokelewa na Mwenyeji wake, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainab Kawawa, ilikua na lengo la kuhamasisha Wananchi kushiriki kikamilifu kuchangia ujenzi wa madarasa katika Shule za Sekondari za Kata, Wilayani Bagamoyo, ili wanafunzi waliochaguliwa awamu ya pili kujiunga na elimu ya Sekondari kuhakikishiwa nafasi ya kujiunga na elimu hiyo.

Akizungumza na Wananchi katika Mkutano maalum wa majumuisho ya Ziara hiyo uliofanyika katika Kijiji cha Kongo, kilichopo Kata ya Yombo Wilayani hapa, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Eng. Evarist Ndikilo amewaasa Wananchi kuacha kuisusia Serikali kujenga miundombinu ya elimu kwa kisingizio cha elimu bure.

Akifafanua Mhe. Eng. Ndikilo amesema kuwa dhana ya elimu bila malipo haimaanishi Wazazi kutochangia kabisa gharama za elimu, bali Serikali inampunguzia mzazi gharama hizo kwa kumlipia mwanafunzi ada, chakula kwa wanafunzi wa bweni pamoja na gharama zingine za uendeshaji wa Shule lakini ujenzi wa miundombinu kama madarasa na madawati ni wajibu wa kila Mwananchi kuchangia ili wanafunzi wapate mahala pa kujifunzia na pale Wananchi wanapofanya vizuri katika ujenzi wa miundombinu, basi Serikali huunga mkono juhudi hizo za Wananchi.

“Nawaagiza Wakuu wote wa Wilaya za Mkoa wa Pwani na Wakurugenzi wote wa Halmashauri wahakikishe Wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari wanapata nafasi hiyo, hususani wale waliochaguliwa awamu ya pili, fanyeni jitihada za makusudi kukamilisha vyumba vya madarasa vinavyoendelea kujengwa sasa ili Wanafunzi hao wapate nafasi ya kuendelea na elimu ya Sekondari” Amesema Ndikilo.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mhe. Zainab Kawawa akitoa takwimu za ufaulu wa kidato cha kwanza kiwilaya, amesema jumla ya Wanafunzi 1869 walichaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari kwa Mwaka 2019 katika awamu ya kwanza, na awamu ya pili jumla ya Wanafunzi 482 wamechaguliwa huku Wilaya ya Bagamoyo ikiwa na upungufu wa vyumba 32 vya madarasa hadi sasa.

Pamoja na uhamasishaji huo wa Wananchi kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa, Mkuu wa Mkoa pia ametumia Ziara hiyo kukagua na kutembelea miradi ya maendeleo ya Sekta ya miundo mbinu ya barabara, Afya na shughuli za wanufaika wa TASAF, ambapo amekagua ujenzi wa mfereji wenye ukubwa wa mita 500, mradi uliotekelezwa na wakala wa barabara vijijini (TARURA) katika Kata ya Dunda, Ujenzi wa Kituo cha Afya Matimbwa, Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Mapinga katika Kata ya Mapinga na Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na Ofisi moja ya Walimu katika Shule ya Sekondari Hassanal Damji, iliyopo Kata ya Magomeni.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • WAPENI ELIMU WANANCHI KUHUSU UGOJWA WA MPOX...

    March 17, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo