• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

MRATIBU WA MRADI WA MARCOSIO TAFIRI AONGOZA WASHIRIKI WA WARSHA KUTEMBELEA WAVUVI WILAYA YA BAGAMOYO...

Posted on: May 29th, 2025

 

Mratibu wa Mradi wa MarCOSIO kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Happy K. Peter, ameongoza timu ya washiriki wa warsha ya MarCOSIO katika ziara maalum wilayani Bagamoyo, ikiwa ni sehemu ya siku ya nne ya warsha hiyo inayowakutanisha wataalamu mbalimbali wa masuala ya bahari na uvuvi kutoka barani Afrika.

Warsha hiyo imewakutanisha washiriki kutoka zaidi ya nchi tisa za Afrika, zikiwemo Namibia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Comoro, Msumbiji, Afrika Kusini, na Ghana. Katika ziara hiyo, washiriki walitembelea ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya ya Bagamoyo, Bw Shauri Selenda, kwa lengo la kujitambulisha rasmi na kueleza madhumuni ya ziara yao wilayani humo.

Bw Selenda aliipongeza TAFIRI kwa kuandaa warsha hiyo na kuichagua Bagamoyo kama sehemu ya mafunzo ya vitendo kwa washiriki. Alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imejipanga kikamilifu kuendeleza sekta ya uvuvi na kuimarisha uchumi wa buluu. Aidha, alibainisha kuwa Soko la Samaki la Bagamoyo ni la pili kwa ukubwa nchini baada ya lile la Feri jijini Dar es Salaam, na Halmashauri imejipanga vyema katika kuhudumia wananchi, hususan wavuvi.

Kwa upande wake, Dkt. Happy K. Peter alisema kuwa ziara hiyo inalenga kuwapa washiriki uzoefu wa moja kwa moja kuhusu shughuli za uvuvi na mazingira ya pwani ya Tanzania. Pia, washiriki walipata fursa ya kutembelea maeneo ya kihistoria yaliyohusiana na biashara ya pembe za ndovu na utumwa katika kipindi cha ukoloni, ikiwa ni sehemu ya kujifunza historia ya eneo hilo.

Aidha washiriki hao waliwatembelea na wavuvi wa Bagamoyo na kushuhudia maisha yao ya kila siku pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo. Hii ni sehemu ya juhudi za mradi wa MarCOSIO katika kukuza uelewa wa pamoja juu ya matumizi endelevu ya rasilimali za bahari na utunzaji wa mazingira ya pwani kwa maendeleo jumuishi ya jamii za ukanda wa bahari.


 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRATIBU WA MRADI WA MARCOSIO TAFIRI AONGOZA WASHIRIKI WA WARSHA KUTEMBELEA WAVUVI WILAYA YA BAGAMOYO...

    May 29, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI...

    May 23, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA UCHAGUZI AKAGUA MWENENDO WA UANDIKISHAJI...

    May 18, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA MAZUNGUMZO NA BODI YA UTALII..

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo