• Malalamiko |
    • Wasilina nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Ushauri |
Bagamoyo District Council
Bagamoyo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Muundo wa Taasisi
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Divisheni na Vitengo
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha TASAF
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Usimamizi wa Usafi na Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Uifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha mawasiliano Serikalini
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Matangazo
    • Miongozo
    • Fomu mbali mbali
    • Mpango Mkakati
    • Bajeti Kuu ya Halmashauri 2024-2025
      • Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Miradi inayoendelea
  • Utalii
    • Kaole Snake Park
    • Kaole Mamba Ranch
    • Caravan Serai
  • Zabuni
    • ZABUNI MBALIMBALI ZA UWAKALA
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao vya Kisheria
    • Vikao vya Wahe. Madiwani
    • Ratiba

MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MRADI WA BIL44.6.

Posted on: May 9th, 2022

Mradi mkubwa wa ujenzi wa mabwawa ya ufugaji samaki TANLAPIA Ltd, uliopo Nianjema ,Bagamoyo, Mkoani Pwani ukikamilika unalenga kusaidia wafugaji wa samaki aina ya Sato nchini na Ukanda wa Sahara , kwani utatumia teknolojia ya kisasa kuongeza uzalishaji na kupunguza athari za Mazingira.

Mradi huo wa kimkakati unatarajia kugharimu dollar milioni 19 sawa na sh.Bilioni 44.6 fedha ya kitanzania Hadi kukamilika kwake.

Akisoma taarifa kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahir Geraruma, wakati alipoweka jiwe la msingi kwenye mradi huo ,Meneja wa Mradi ,Farida Bozohera alisema ,Hadi kufikia mwezi April mwaka huu mradi umeshatumia sh.bilioni 11.5 .

"Mradi huu ukikamilika tutatumia teknolojia ya kisasa inayolenga kuongeza uzalishaji na kupunguza athari za Mazingira, kwa wafugaji wa samaki aina ya sato katika nchi zilizo Kusini mwa Ukanda wa Sahara.:;"alisema Farida.

Awali akipokea Mwenge huo ukitokea Halmashauri ya Chalinze, kwenye viwanja vya shule ya msingi Fukayose, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Shauri Selenda alisema, Jumla ya miradi 11 yenye thamani ya sh.Bilioni 46.308.2 katika kata nne imetembelewa.

Nae Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallah alieleza ,miradi 25 yenye thamani ya Bilioni 47.2 imepitiwa na mwenge huo katika Halmashauri mbili za wilaya hiyo.

Alieleza ,wilaya hiyo ina Halmashauri hizo mbili ambapo Halmashauri ya Chalinze imetembelewa miradi 14 iliyogharimu milioni 937.8 na Bagamoyo miradi 11 yenye thamani ya Bilioni 46.3.

Akielezea kuhusu mradi huo wa ufugaji samaki Zainab alibainisha ,Ni uwekezaji mkubwa katika Halmashauri ya Bagamoyo, Afrika Mashariki na kati na Ukanda wa Sahara.

Miradi mingine iliyopitiwa ni pamoja na mradi wa upanuzi wa maji kijiji cha Fukayose, kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la upasuaji na wodi ya wazazi na barabara kiwango cha Pavement blocks mita 880.

Mwenge wa Uhuru uliingia Mkoani Pwani,"; Mei mosi na kutembelea miradi 111 yenye thamani ya sh.Bilioni 69.2 ,kwenye Halmashauri Tisa ambapo Mei 10 mkoa huu utaukabidhi Mwenge huo Jijini la Dar es Salaam.

Miradi mingine iliyotembelewa katika Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru ni Mradi wa Maji uliopo katika Kata ya Fukayosi unatao hudumia Wananchi wa kitongoji cha Fukayosi,Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Fukayosi,Mradi wa Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa shule ya sekondari Hassanal Damji,Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Bamani iliyopo kata ya Dunda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 AWAMU YA PILI... May 09, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU WILAYA YA BAGAMOYO... February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA YA OBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.. February 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI... July 14, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAPANDA MITI 500 ENEO LA MNADA WA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA...

    April 15, 2025
  • TUTAENDELEA KUSIMAMIA KWA DHATI NA HAKI MISINGI YA DEMOKRASIA...

    April 02, 2025
  • ELIMU KUHUSU MPOX YATOLEWA KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI...

    March 20, 2025
  • WAPENI ELIMU WANANCHI KUHUSU UGOJWA WA MPOX...

    March 17, 2025
  • Angalia zote

Video

SOKO LA SAMAKI BAGAMOYO.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Instagram

Tovuti muhimu

  • Salary Slip Portal
  • Presidential Office Regional Administrative and Local Goverment
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Muongozo wa Ramani

Wasilina nasi

    Bagamoyo

    Anwani ya Posta: Box 59 BAGAMOYO

    Simu: 0733860575

    Simu ya kiganjani: 0733860575

    Barua pepe: ded.bagamoyo@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo